Huduma ya MGMT,haina masharti magumu ya kujiunga,unatakiwa kufanya mambo yafuatayo:
Maombi
Mwombe Mungu akupe kibali cha kujiunga na huduma hii, kwani kuna watu wengi wamejiunga kwa kutumia akili zao, wamefika njiani mazingira yamewashinda,wameondoka bila kuaga.
Hakikisha unao wito moyoni mwako ambao utausimamia katika huduma. Jambo hili litakufanya usimwangalie mwanadamu, masilahi,kunung'unika au kuilalamikia,huduma badala yake utamtazama Mungu aliyekuita kupitia kwenye hii huduma na utamuuliza jambo la kufanya kila wakati.
Ni vema zaidi kama utakuwa UMEOKOKA na usiwe mtu wa dini, kwani huduma hii hufanya kazi na makanisa mbalimbali bila kugusa mapokeo ya dini "za watu" zaidi ya kumtangaza Kristo….sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa…1Kor 1:23
Michango ya pesa
Unaweza kutuma fedha kwa kuleta katika ofisi zetu zilizopo
THE MINISTRY OF GOD'S MESSAGE TANZANIA,
S.L.P. 12271, ARUSHA
OFFICE:OTTU BUILDING,ROOM NO 132 & 133 BLOCK "B" Ist FLOOR.
TEL: +255-027-250-1971, +255-0784-517603, 0715-517603, 0759-357561.
E-mail:info@mosesmalugu.org
Au tuma kwa njia ya Bank ya CRDB tawi la Arusha kwa anwani ifuatayo:
Account Name: THE MINISTRY OF GOD’S MESSAGE TANZANIA
Country: TANZANIA
Bank: CRDB PLC
Branch: ARUSHA
A/C NO: 01J2034029100
SWIFT CODE: CORU TZ TZ.
au kwa njia zingine kama western union, moneygram nk. (tafadhali wasiliana nasi kama umeamua kutuma kwa njia hii)
Web www.mosesmalugu.org
Kujitolea
Unaweza kushiriki pia kwa njia ya kujitolea "volunteer", kutoa "zawadi" kwenye huduma au kwa njia ya sadaka ya shukrani mbele za Mungu.Lakini pia unaweza kutuma fedha kwa njia ya Bank ya CRDB tawi la Arusha kwa anwani ifuatayo:
Kujiunga kwa kujitolea (volunteer) kwa njia ya:
Kuwa na kujenga uhusiano (Partinaship) kati ya huduma yetu na nyingine
Kutunza yatima,wajane,waathirika wa ukimwi,masikini,n.k,
Kufundisha mashule ya vijijini
Kujitolea kufanya kazi na huduma ya MGMT ili kufikisha malengo na makusudi yake.
Zawadi
Aina ya zawadi utakazoweza kuzituma:
Usafiri kwa maana ya gari( hasa Toyota L/Cruiser 4 wheel drive)
Nguo, Biblia na vitabu vingine
Vyombo vya kuhubiria na mashine (projector) ya kuendeshea sinema,
Computer (laptop) au yeyote,
Printer, video na digital camera,